sombe

Sombe

"Unapotayarisha sombe, ni muhimu kuhakikisha tunapata pia vitafunio ili tupate virutubisho vyote muhimu... Ikiwa unayo sombe, unaweza kuwa na samaki au nyama kama vitafunio. Kwa sababu hapa tunapata chuma, na kwenye nyama tunapata protini."

“When you cook sombe, we have to make sure we also have sides so that we have all the essential nutrients.... If you have sombe you’re either going to have fish or you’re going to have meat on the side. Because in here we have iron and in here--in the meat we have protein.”

Viungo / Ingredients

  • Majani ya muhogo yaliyohifadhiwa kwa baridi / Frozen cassava leaves
  • Karoti ya manjani / Celery
  • Pupu / Leek
  • Biringanya / Eggplant
  • Pilipili ya kijani / Green pepper
  • Vikombe 2 vya mafuta ya ufuta au mafuta ya njugu / 2 cups palm oil or canola oil
  • Chumvi / Salt
  • Kitunguu sumu (hiari) / Garlic (optional)
  • Spinachi (hiari) / Spinach (optional)

Maelekezo / Instructions

 1.  Tiya maji kwenye sufuria hadi ichemke, kisha ongeza majani ya muhogo (sombe). "Kwa sababu tunanunua hii dukani, hatujui jinsi wanavyoipika. Kwa hivyo, tunachemsha maji kama tunavyofanya sasa. Unafungua pakiti na kuweka sombe ndani na kuchemsha na kuondoa harufu mbaya."

2.  "Wakati inachemka, osha mboga hizi zote." Osha na kata celery, leek, pilipili kijani, na bilinganya. "Ikiwa bilinganya ni mpya, kata pamoja na ngozi yake. Ikiwa sio mpya, ondoa ngozi yake."

3. Weka mboga zilizokatwa, mafuta, na chumvi kwenye sufuria pamoja na sombe. "Baadhi ya watu hutumia vitunguu sumu... Kwa sababu mboga hizi zinasaidia kufanya sombe kuwa laini, unaweza pia kuongeza spinachi ikiwa unataka... Spinachi husaidia kufanya iwe laini zaidi." 

4. "Mchakato mzima unachukua masaa mawili ili sombe ipikike kabisa." Koroga mara kwa mara wakati inapika.

5. "Baada ya sombe au majani ya muhogo kuiva kabisa, unaweza kuongeza karanga iliyosagwa, au samaki, au mifupa. Ni chaguo lako... lakini usichanganye kila kitu Pamoja."

6. Tumikia na ugali na samaki au nyama. "Unaweza kula na ugali au fufu. Unaweza kula na ndizi au wali au kitu kingine chochote."



Laurence
ImageImageImage